2017-01-27 16:55:00

Baba Mtakatifu anasema tufanye shukrani ya kumbukumbu ya maisha


Kwenye somo la liturjia ya  siku kutoka katika kitabu cha Wahebrania ,ni mambo matatu ya kutazama katika kuishi maisha ya kikristo  kwa kutazama wakati ulio pita , uliopo na ujao. Na zaidi tunaitwa kufanya kumbukumbu, kwasababu maisha ya kikristo hayakuanza leo , bali yanaelendelea . Kufanya kukmbukumbu ni kukumbuka kila kitu kwa yale mambo mema na yale yasiyo mema , na kutengenza historia , mbele ya Mungu bila kuifunika na kuificha.
Ni maneno ya Baba Mtakatifu Francisko wakati wa Misa Takatifu Ijumaa 27 Januari 2017 katika Kikanisa cha Mtakatifu martha Mjini vatican, akisema ndugu zangu  tufanye kumbukumbu za wakati ule wa mwanzo, kwani ni siku za furaha , za kuendelea mbele katika imani  na hasa  unapoanza kuishi kwa imani, nakatika  mateso ya majaribu. Huwezi kutambua maisha ya kikristo ,maisha ya kila siku ya  kiroho  bila kuwa na kumbukumbu.


Anasisitiza na siyo tu kutotambua , bali huwezi kuishi maisha ya kikristo bila kuwa na kumbukumbu ya ukombozi  wa Mungu katika maisha  yangu, kumbukumbu ya majanga yangu ya maisha , na ni  jinsi gani Mungu ameniepusha na majanga hayo.Kumbukumbu ni neema , ya kuomba  ili  Bwana aweze kusahau  yaliyopita , na hata mimi pia ni sisahau kipindi kile kizuri  au kibaya ; furaha na mateso ya misalaba . kwa njia hiyo mkristo ni mtu wa kumbukumbu.
Anaendelea kufafanua akisema ,Mwandishi wa barua hiyo anatufanya tuelewe kwamba sisi sote tuko safari ya matarajio ya jambo flani, ambapo itafikia kikomo cha kukutana ,yaani kukutana na Bwana,anatuhimiza tushi kwa imani.Matumaini utazama wakati endelevu , kwa njia hiyo haiwezekani mkristo kuishi bila kuwa na kumbukumbu za mambo yaliyotendeka , haiwezekani mkriso kuishi maisha yake bila kutazama wakati endelevu kwa matumaini ya kukutana na Bwana.


Baba Mtakatifu anasisitiza kwamba Yeye anasema sentensi nzuri ya kwamba “ Bado muda kidogo , na hivyo Maisha ni kama upepo maana yanapita.Anatoa mfano kwamba mtu akiwa kijana ufikiria bado anao muda mrefu , lakini maisha tanatufundisha japokuwa  ni maneno yasemwayo na kila mmoja ya kwamba tazama muda ulivyo pita! namjua tangu utoto na sasa anaoa! Hama kweli muda unapita kwa haraka.Lakini matumaini ya kukutana na Bwana ni mvutano kati ya kumbukumbu na matumaini , wakati uliopita na endelevu.
Hali kadhalika barua inatualika kuishi wakati uliopo ,japokuwa   mara nyingi  kuna machungu na mateso ,ujasiiri na uvumilivu: yaani, tunapaswa  kusema ukweli, bila aibu,  kuvumiliana katika maisha : sisi ni wadhambi Baba Mtakatifu anasisitiza aliye wa kwanza na hatakayekuja  baadaye , maana hatuwezi kufanya orodha , kwasababu wote tu wadhambi.Wote tunakwenda mbele kwa ujasiri na uvumilivu . Sio kubaki tumesimama kwani kusimama hakutuwezeshi kukua.


Hatimaye mwandishi wa Waebrania natuhimiza tusitende dhambi , ambayo huzuia  kuwa na kumbukumu, matumaini, ujasiri  na uvumilivu.Woga ni dhambi inayokuzuia usiende mbele kutokana na hofu uliyo nayo wakati Yesu anatueleza “ msiogope “walio na hofu mara nyingi ubaki nyuma kwa kufunga wao wenyewe kuotokana na woga huo.
Usije hatarisha tafadhali, Baba Mataktafi anasema  bali uwe na taadhali, kwani kuna matumaini kwa kila mtu , usiache ugandizwa na ukasahau hata neema nyingi ulizopokea .Hofuinakuondolea matumaini ya kuendelea mbele .Mkristo unapaswa kuishi wakati uliopo na tayari bali usiwe na sawa na mtu anapokuwa njiani , mvua ikaanza kunyesha wakati nguo aliyo  vaa siyo nzuri ikajikunyata yote na kumbana, hiyo inaelezea juu ya mioyo yenye kujikunyata yenyewe , iliyo na woga kwani hiyo ni dhambi dhidi ya kumbukumbu , ujasiri, uvumilivu na matumaini.Bwana atusaidie kukuza kumbukumbu , matumaini , na atupatie kila siku ujasiri na uvumilivu, atuondolee ule woga unao tufanya tuwe na hofu ya kila kitu , mioyo iliyo fungwa , migumu wakati Yesu mwenyewe anasema anaye hifadhi maisha yake mwenyewe atapoteza.

Sr Angela Rwezaula 

Idhaa ya Kiswahili ya Radio vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.