2017-03-01 15:01:00

Mchango kwa ajili ya ukarabati wa Makanisa Makuu nchini Palestina


Vatican itatoa mchango mkubwa kwa kuchangia shughuli zinazoendelea za ukarabati wa Kanisa la Kaburi Takatifu Yerusalem na Kanisa Kuu alipozaliwa Bwana wetu Yesu Bethlehemu . Hayo yamethibitishwa na Issa Amil Kassissieh   Balozi mwakilishi wa nchi ya Palestina nchini Vatican katika Shirika la Habari la Fides. Nia ya Vatican kufanya hivyo pia ilimethibitishwa kwenye ofisi za ubalozi na Kardinali Leonardo Sandri , Rais wa Baraza la Kipapa kwa Makanisa ya nchi za Mashariki , kwenye mkutano wao uliofanyika tarehe 27 Februari 2017 mjini Vatican.

Chini ya usimamizi wa Ndugu wadogo wa Mtakatifu Francisko wa Assisi , wanaotunza maeneo matakatifu huko Yerusalem,Balozi anasema watawatangazia ni kiasi gani cha mchango na utaratibu upi utumike kuwafikia kiasi hicho, anaongeza; kwa sasa, kwa niaba ya Rais wa nchi ya Palestina , Mahmud Abbas na watu wote wa Palestina ninatoa shukrani kwa Vatican katika juhudi zao kuendelea kusimamia katika kuleta haki na mani kwa nchi Takatifu,ambayo ni maeneo  aliyozaliwa na kusulibiwa Bwana wetu Yesu kristo. 
Ukarabati wa Kanisa kuu ya Kuzaliwa kwa Bwana wetu Yesu Kristo huko Bethlehemu ulianza mwaka 2013, unaoshirikisha  Jumuiya tatu za kidini ambazo ni Jumuiya ya Waorthodox wa kigiriki, Waarmenia na Wafranciskani ambao ndiyo wapo ni wasimamizi wa Kanisa Ku una hawa,ndiyo wenye haki na usimamizi wa mali ya Kanisa  kwa mujibu wa katiba ya Status Quo.

Kwa upande wa kazi ya ukarabati  wa Maktaba ya Kanisa la  kaburi  Takatifu ulianza Mei 8 2016.Pamoja na hayo Mpango wa ukarabati wa Kanisa la kaburi Takatifu unatakiwa gharamia dola milioni 3.3 ambazo zitatolewa kwa ushirikiano kutoka Kanisa la Orthodox wa Kigiriki, Kanisa  la Waarmenia na Kanisa Katoliki.Mwezi Aprili 2016 Mfalme wa Joardan Abdallah II alitoa mchango wake binafsi kwa ajili ya mpango huo na  Oktoba mwaka jana Rais Mahmoud Abbas wa Palestina naye pia alitoa mchango binafsi kusaidia  ukarabati wa maktaba ya Kanisa la Kaburi Takatifu.Ndugu wadogo wa Mtakatifu Francisko ambao ni walinzi wa maeneo matakatifu  kwa kupitia njia zake za mawasiliano, mara kwa mara wanatoa taarifa rasmi juu ya maendeleo ya kazi inayoendelea.


Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.